
Namba ya mtahiniwa …………………………...
(c) Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata:
Mwanafunzi ikibali, mbele ya wako mwalimu.
Katika siku si mbali, utakuwa aalimu.
Kijitia baradhuli, baadaye ulaumu,
Mbele ya wako mwalimu, mwanafunzi ikibali.
Usijifanye kiburi, kujifanya chakaramu.
Hiyo wanaita shari, ndani yake ina sumu,
Hivi hauna habari, heshima kitu adimu,
Mbele ya wako mwalimu, mwanafunzi ikibali.
Katika hii sayari, namba moja ni elimu,
Usiipate sufuri, kisha hapo ulaumu,
Maisha haya safari, mwana ujenge timamu,
Mbele ya wako mwalimu, mwanafunzi ikibali.
Katika hii sayari, namba moja ni elimu,
Usiipate sufuri, kisha hapo ulamu,
Maisha haya safari, mwana ujenge timamu,
Mbele ya wako mwalimu, mwanafunzi ikibali.
Ni walezi mashuhuri, hivyo wana umuhimu,
Wameishika nambari kutokana na kalamu,
Usimwendeshe chuchuri, uidumishe nidhamu,
Mbele ya wako mwalimu, mwanafunzi ikibali.
Mwalimu baba na mama, hilo wazi ufahamu
Hivyo tazama ndarama, zisisababishe ghamu,
Neno hili la zama, shika nakupa jukumu,
Mbele ya wako mwalimu, mwanafunzi ikibali.
Sitapenda kukuchosha, kwa mengi kukushutumu,
Nakutakia maisha, ya hsule yenye utamu,
Ili upate bashasha, na mema kutakadamu,
Mbele ya wako mwalimu, mwanafunzi ikibali.
(i) Mtunzi wa shairi hili anatoa ujumbe gani?