
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org
SEHEMU B (Alama 40)
Jibu maswali yotekatika sehemu hii.
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org
3. Ainisha maneno yaliyokolezwa wino katika tungo zifuatazo:
(i) Wangapiwaliondoka mapema leo?
(ii) Wachezaji wangapiwatashiriki kwenye mechi ya kwanza?
(iii) Wanangu wapendwa niwaeleze mara ngapimpate kunielewa?
(iv) Wawakilishi wote waliungamkono hoja ya mbunge wa Kusini Unguja.
4. Eleza kwa ufupi mazingira manne ambayo kielezi huweza kujipambanua, kisha tunga sentensi moja
kwa kila aina ya mazingira.
5. Eleza maana mbili kwa kila tungo zifuatazo:
(a) Mama anaota.
(b) Tafadhali nipe sahani ya kulia.
(c) Vijakazi wanalima barabara.
(d) Amekanyaga mtoto.
6. Kwa kutumia mifano kutoka katika riwaya ya Takadiniliyoandikwa na Ben J. Hanson (MBS), eleza
kwa kifupi madhara manne yanayoweza kutokea katika jamii iwapo itaendekeza mila potofu ya
kuwabagua walemavu wa ngozi.
7. Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata katika kijitabu cha kujibia.
Chawa huyo ni kinyozi, mtia wembe kichwani,
Ndiye huharibu ngozi, anapokata fashini, Chawa
ni huyo mkazi, uliyenaye jirani, Usimdhanie
mbuzi, huyo yuko majanini, Wala usidhani
funzi, umuonaye shambani, Hawa hawana ujuzi,
wa kukunyoa mtani, Panapouma ufizi, sumu
hutoka kinywani, Wapi hutokea nzi, kama si
pako chooni, Chawa aliye kichwani, ni huyo
kinyozi wako.
Chawa unapomuona, upesi muweke dole,
Usimwache kunona, mpaka azue kelele,
Jitahidi kumbana, akatokomee mbele,
Ukimwacha kutuna, atakutia upele, Usije
kula dona, na katafuta mchele, Chawa
usimpe jina, abaki akutawale, Ukianza
kujikuna, mtafute kwenye nywele, Na nguoni
hujibana, mkame kama nyenyele, Chawa
aliye kichwani, ni huyo kinyozi wako.
Maswali
(a) Kwa kutumia mfano, fafanua mtindo uliotumika katika shairi hili kwa kutoa hoja mbili.
Ukurasa wa 4 kati ya 5