
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org
SEHEMU A (Alama 15)
Jibu maswali yotekatika sehemu hii.
1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo katika
kijitabu chako cha kujibia.
(i) Neno lipi kati ya maneno haya linaweza kudokeza mtenda au mtendwa?
A Kiunganishi B Kivumishi C Kihisishi D Kiwakilishi
E Kielezi
(ii) Ni sentensi ipi hainakitenzi kisaidizi?
A Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa mtiifu. B
Watoto wanatakiwa kulala mapema ili wawahi shuleni. C
Paka alikuwa anataka kula chakula cha mbwa.
D Juma alikuwa anasoma kitabu cha hadithi za mapenzi.
E Robert Kelly anataka kuja kutumbuiza mwezi Desemba.
(iii) Ni seti ipi inawakilisha kikamilifu wahusika wa fasihi simulizi? A
Vitu, mahali, wanyama, binadamu, fanani na maleba.
B Hadhira, wanyama, maleba, binadamu na fanani.
C Hadhira, binadamu, wanyama, vitu, mahali na fanani. D
Fanani, vitu, mahali, binadamu, maleba na wanyama.
E Wanyama, manju, binadamu, vitu, mahali na maleba.
(iv) Bainisha seti ya maneno inayofaa kuingizwa kwenye kamusi kwa kuzingatia mpangilio wa
alfabeti.
A Jabali, jadhibika, jabiri, jadi, jalada B
Jabali, jabiri, jadhibika, jadi, jalada C
Jabali, jadi, jadhibika, jalada, jabiri D
Jabiri, jabali, jalada, jadi, jadhibika
E Jabali, jalada, jabiri, jadhibika, jadi
(v) Ni sifa ipi haitofautishi fasihi simulizi na fasihi andishi?
A Ukubwa B Uhifadhi C Uwasilishaji D Ukuaji
E Ueneaji
(vi) Jozi ipi ina vipengele sahihi vinavyounda umbo la ndani la kazi ya fasihi
simulizi? A Falsafa, muundo, ujumbe, wahusika
B Mandhari, msimamo, ujumbe, dhamira C
Ujumbe, mtazamo, migogoro, dhamira D
Ujumbe, msimamo, dhamira, wahusika
E Lugha, mgogoro, falsafa, mtindo
Ukurasa wa 2 kati ya 6