Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA MTIHANI WA KUHITIMU KIDATO CHA NNE 021 KISWAHILI (Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni) Muda: Saa 3:00 Jumatatu, 05 Novemba 2018 asubuhi Maelekezo 1. Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E zenye jumla ya maswali kumi na tano (15). 2. Jibu maswali yote katika sehemu A, B na D, swali moja (1)kutoka sehemu C na maswali matatu (3)kutoka sehemu E. Swali la 15ni lazima. 3. Zingatia maagizo ya kila sehemuna ya kila swali. 4. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa haziruhusiwikatika chumba cha mtihani. 5. Andika Namba yako ya Mtihanikatika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia. Ukurasa wa 1 kati ya 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org SEHEMU A (Alama 10) UFAHAMU Jibu maswali yotekatika sehemu hii. 1. Soma kwa umakini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata. Ingawa utaona kuwa haya nitakayoyasimulia hayakuhusu ndewe wala sikio, kwa vile mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi, lakini kumbuka, mwenzio akinyolewa na wewe tia maji maana yaliyompata beku na ungo yatampata. Ukiona yale yanayomsibu Mwanaheri hivi sasa ni dhahiri utakubaliana na mimi kuwa ujana ni kama maua. Kwa matatizo anayoyapata Mwanaheri ni kuntu kuwa upigao ndio ufunzao. Ingawa kwake ni sawa na maji yaliyomwagika hayazoleki, na ninaamini kuwa kwa wengine hili ni fundisho kwa kuwa watu husema, kama hujui kufa tazama kaburi. Uzee unaomkabili Mwanaheri sasa unahitaji msaada mkubwa wa mtoto wake haidhuru mjukuu wake. Lakini maskini, hakupenda watu hao kuwa nao tangu awali ya maisha yake. Ingawa hivi sasa anao watoto wa ndugu zake, lakini hawana msaada wowote kwake. Nidyo maana watu hawakukosea kusema ndugu akizaa na wewe uzae maana changu si chetu. Hata wale mashoga zake waliokuwa wakishirikiana naye katika kukata mitaa, wamemtupa Kigoma mwisho wa reli. Kwa uzuri, alhamdulillah, aliumbika, maana alikuwa chuma hasa wala si masihara. Enzi zake Mwanaheri, alikuwa Mwanaheri kweli. Alikuwa hapitwi na mwanamume. Mbali ya kuwa na kidevu cha mfuto chenye kidimbwi kwa mbali, macho yake ya gololi yalimvuta mwanamume yeyote hata muumini wa dini. Miguu iliumbwa kadri ya mwili wake. Ukimwangalia kwa nyuma umbo lake ni sawa na umbo la namba nane. Ingawa alikuwa na nywele za kipilipili, lakini alizitengeneza zikawa kama za singa. Uzuri wote huo aliotunukiwa kama hedaya yake hapa duniani, umeathiriwa na mwenendo tu. Mwenendo huu ulimpa jina baya la kuitwa jamvi la wageni. Mwenendo huu ulikuwa sadfa ya ambacho kimekamilisha ule usemi wa wahenga kuwa uzuri wa kuyu ndani imeoza au uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti. Alipokuwa kijana alikuwa hapendi wachumba, wala watoto kwa kuchelea kutibua starehe zake. Kwa jinsi alivyokuwa anadanganyika na ujana pamorja na rangi za dunia akifikiri atakuwa kijana mpaka kufa kwake. Alijididimiza katika wimbi la starehe hadi akazama kiasi kwamba akalowana chapa. Naam! aliyetota hajui kutota. Mbali na kutosikia la baba wala la mama, pia hakusikia la viongozi wa dini. Maisha yalikuwa dunia na yeye na dunia. Ingawa alikuwa na wenzake katika shughuli hizo, lakini ni yale yale, yetu yetu, yakikupata yako peke yako, lakini wenzako walikuwa wakifanya hayo na akili zao. Yeye hakukumbuka kwamba nahodha mtweka chombo si mjinga wa bahari kwani mtu hufanya jambo kwa akili zake, lakini Mwanaheri mwenzangu na miye hakuwa na hili wala lile. Wenzake hao sasa wana watoto wao ambao wanawasaidia kwa moja au kwa jingine, wakati yeye anaumbuka. Kidagaa kimemwozea. Mbali ya kuwa na ubao mara kwa mara, pa kuweka ubavu pia alipakiskia kwenye bomba. Kwa mtu aliyeuona ujana wa Mwanaheri, hawezi kuamini kuwa ni huyu anayeahirika sasa hivi. Naam! Asiyesikia la mkuu huvunjika guu, kama wanenvyo waneni, asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu. Ukurasa wa 2 kati ya 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org Majutu ni mjukuu, na hivi sasa nina imani kuwa Mwanaheri anajuta kwa kuuchezea ujana wake. Hakujua ujana ni hazina kubwa ya maisha ya baadaye. Hivi sasa ninahisi angalipenda arudie hali ileile ya juzi na jana ili apate mume yeyote yule, hata angalikuwa kabwela kupindukia, mbali ya wale wa maana aliokuwa akiwapiga mateke. Hata hivyo, yote haya ni kutaka kupata mtoto, hata liwe toto jinga, maana jinga ni lako, kwani tikiti baya lipo shambani kwako. Lakini hilo ni jambo ambalo haliwezekani hata afanye ibada usiku na mchana. Hata hivyo, afae hakosi mzishi, kwani ingawa watu wrengi wamekata mguu, kuja kumliwaza, bado ndugu wachache hufika kumhudumia, angalau kwa kujitoa kimasomaso. Watu husema, damu nzito kuliko maji. Maswali (a) Kwa mujibu wa habari uliyosoma eleza kitu kilichoathiri uzuri wa Mwanaheri. (b) Andika nahau mbili zinazopatikana katika kifungu cha habari ulichokisoma. (c) Fafanua methali zifuatazo kwa kutoa mifano halisi kutoka katika simulizi uliyosoma: (i) Maji yakimwagika hayazoleki. (ii) Asiyesikia la mkuu huvujika guu. (d) Andika kichwa cha habari kinachofaa kwa habari uliyosoma. 2. Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasipungua mia moja (100). SEHEMU B (Alama 25) SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA Jibu maswali yotekatika sehemu hii. Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org 3. Fafanua dhana zifuatazo na kisha toa mfano mmoja kwa kila dhana uliyofafanua. (a) Neno (b) Kirai (c) Kishazi (d) Sentensi (e) Kamusi 4. Nyambua maneno yafuatayo ili kupata maneno mawikli zaidi kwa kila neno; (a) beba (b) pokea (c) rudi (d) soma (e) shughuli (f) sema (g) penda (h) heshima (i) pigo (j) pika Ukurasa wa 3 kati ya 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org 5. Bainisha tabia za maumbo yaliyokolezwa wino katika vitenzi ulivyopewa. (a) Futaubao. (b) Hutafaulu mtihani. (c) Ametualika. (d) Mtoto hulia mara nyingi. (e) Yeye nimwalimu. (f) Mgonjwa amejilaza chini. (g) Wanavisoma vitabu vyao. (h) Paka amepigwa. (i) Mti umekatika. 6. (a) Eleza maana na dhima ya kiunganishi katika sentensi. (b) Tunga sentensi mbili kwa kila kiunganishi kifuatacho; (i) kwa sababu (ii) kamba (iii) ingawa (iv) lakini 7. “Kuambatanisha maneno ni namna mojawapo ya kuzalisha maneno mapya katika lugha ya Kiswahili.” Bainisha njia tatu za kuambatanisha maneno kisha toa mifano miwili kwa kila njia uliyobainisha. SEHEMU C (Alama 10) UANDISHI Jibu swali moja (1)kutoka sehemu hii. 8. Tofautisha muundo wa barua rasmi na barua za kindugu/kirafiki. 9. Jifanye kuwa mfanyabiashara wa mchele na unataka kuitangaza biashara yako nje na ndani ya nchi. Andika tangazo kuhusu biashara hiyo na jina lako liwe Pera Mlavi. SEHEMU D (Alama 10) MAENDELEO YA KISWAHILI Jibu swali la kumi (10) 10. “Sifa ya lugha ni kuwa na uwezo wa kupokea msamiati kutoka lugha za kigeni.” Kwa kutumia mifano, eleza sababu nne zilizokifanya Kiswahili kuwa nameno mengi ya Kiarabu kuliko kutoka lugha nyingine za kigeni. Ukurasa wa 4 kati ya 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org SEHEMU E (Alama 45) FASIHI KWA UJUMLA Jibu maswali matatu (3)kutoka katika sehemu hii. Swali la 15ni la lazima. ORODHA YA VITABU USHAIRI Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP) Malenga Wapya - TAKILUKI (DUP) Mashairi ya Chekacheka - T.A. Mvungi (EP & D.LTD) RIWAYA Takadini - Ben J. Hanson (MBS) Watoto wa Mama N’tilie - E. Mbogo (H.P) Joka la Mdimu - A.J. Safari (H.P) TAMTHILIYA Orodha - Steve Reynolds (MA) Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe - E. Semzaba (ESC) Kilio Chetu - Medical Aid Foundation (TPH) 11. Eleza maana na matumizi ya methali zifuatazo: (a) Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua. (b) Mchimba kisima huingia mwenyewe. (c) Ukiona zinduna ambari iko nyuma. (d) Waarabu wa pemba wanajuana kwa vilemba. (e) Mbaazi ukikosa maua husingizia jua. 12. “Washairi hutumia mashairi yao kuelimisha jamii kuhusu mambo yanayoikabili.” Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kutumia hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma. 13. “Mwanamke ni mtu mwenye huruma na fadhila.” Thibitisha hoja hiyo kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika vitabu viwili vya riwaya kati ya vilivyoorodheshwa. 14. “Waandishi wa tamthiliya wameshindwa kufikisha ujumbe kwa jamii iliyokusudiwa.” Kanusha kauli hii kwa kutumia joha tatu kwa kila kitabu kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma. 15. Tunga utenzi wenye beti nne (4) juu ya “Umuhimu wa Katiba Mpya Tanzania.” Ukurasa wa 5 kati ya 5