Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA NATIONAL EXAMINATIONSCOUNCIL CERTIFICATE OF SECONDARYEDUCATIONEXAMINATION 021 KISWAHILI (Kwa watahiniwa Waliokona Wasiokuwa Shuleni) Muda: Saa 3 Jumann Maelekezo 1. Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E. 2. Jibu maswali yote katika sehemu A, B na D, swali moja (1) kutoka sehemu C (3) kutoka sehemu E. Swali la 15 ni lazima. 3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na ya kila swali. 4. Simu za mkononi haziruhusiwi katika chumba cha mtihani. 5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibi Ukurasa wa 1 kati ya 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org SEHEMU A (Alama 10) UFAHAMU Jibu maswali yote katika sehemu hii. 1. Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata. Nchi yetu ya Tanzania imejulikana sana kutokana na mazingira yake yanayowavutia watalii. Hali yake ya hewa ni nzuri na yenye kutamanika. Mvua yake si nyingi na haichukizi bali ni ya rasharasha na tena ni ya hapa na pale. Majira yenyewe ya masika ni mafupi sana na hayana baridi kama huko ulaya. Kitu hasa kinachowavutia watalii kutembelea nchi yetu ni pwani zetu ambazo zina mchanga mweupe na laini. Mchanga wenyewe hauna matope wala uchafu wowote. Kandokando ya pwani hizo kuna vichaka vyenye miti yenye rangi chanikiwitina maua ya sampuli nyingi ya kutamanisha. Maua hayo yapo ya rangi nyekundu na vilevile hunukia vizuri, ama huweza kuwa na rangi ya manjano na kisha yakawa mviringo. Kando kidogo unaweza kuona mawe makubwa yenye mapango makubwa mweusi ambamo wanyama wakubwa na wakali kama chui huishi. Pengine hata wanyama wa kuchekesha na hata watundu kama tumbili na kima huonekana humo. Pembezoni, ambapo ni nje ya pwani zetu, kuna mashamba yenye mimea ya rangi ya kijani ikinawiri hasa wakati wa masika. Kipindi hiki wakulima nao huwa wanajishughulisha na matayarisho pamoja na maendeleo ya kazi zao za kila siku. Baadhi yao hupenda kufanya kazi huku wamevaa majoho marefu meupe au pengine shuka za kaniki zilizochakaa. Aidha, wengine hawajishughulishi kamwe na mambo ya mavazi kwani wao huvaa vikoi vikuukuu na vilivyokwajuka, bila kuja Zaidi ya pwani zetu, watalii huvutiwa sana na mbuga zetu za wanyama wa porini. Wengi wa wanyama katika mbuga zetu huwa na gozi zenye madoa ya rangi za kuvutia. Pengine hata maungo yao huwa ya kutisha na yasiyokuwa ya kawaida. Mathalani ukimwona kifaru unadhani amekasirika na kwamba anataka kukurarua vipande vipande. Simba naye anajulikana kwa makucha yake marefu ya kutisha. Kiboko kwa upande wake, anajulikana kwa unene wake. Tumbo lake ni kubwa la kuchekesha kwani kila umwonapo utadhani matumbo yataporomoka dakika yoyote. Basi mambo kama hayo na mengine mengi, ndiyo yanayowavutia watalii kuja kwetu. Watalii hawa ambao wengine kati yao ni warefu na pia wachangamfu lakini wapo walio wembamba na wepesi katika kuipanda milima yetu. Hata hivyo, wapo pia wazee vikongwe wenye ari na nguvu katika kuipanda milima hiyo. Wote hawa wanakuwa na hamu ya kutembelea vivutio vyetu. Baada ya kutembelea sehemu mbalimbali, hurudi kwao na furaha isiyo kipimo huku wakituachia fedha nyingi za kigeni. Ukurasa wa 2 kati ya 5 Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org Maswali (a) Andika kichwa cha habari hii kisichozidi maneno manne. (b) Taja dhamira kuu inayotokana na habari hii. (c) Mwandishi anatoa ushahidi gani kuthibitisha kuwa nchi yetu ina vivutio vingi vya (d) “Wenyeji wa nchi yetu ya Tanzania nao ni sehemu ya vivutio vya utaliThibitis kwa mujibu wa habari uliyosoma (e) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kufungu cha habari (i) Chanikiwiti (ii) Vilivyokwajuka 2. Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyozidi arobaini (40). SEHEMU B (Alama 25) SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA Jibu maswali yote katika sehemu hii. Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org 3. (a) Eleza maana ya utohoaji. (b) Maneno yafuatayo yametoholewa kutoka lugha gani? (i) Picha (ii) Duka (iii) Shule (iv) Rehema (v) Shati (vi) Trekta (vii) Ikulu (viii) Bunge (ix) Achali 4. Taja aina za sentensi zifuatazo kisha eleza muundo ujengao kila sentensi. (a) Maisha ni safari ndefu. (b) Ukisoma kwa bidii utafaulu kwa kiwango cha juu. (c) Mtoto aliyelazwa hospitalini ameruhusiwa kwenda nyumbani. (d) Nitakuja leo ingawa nitachelewa sana. (e) Alinunua madaftari lakini kitabu cha Kiswahili alipewa na mwalimu. 5. (a) Eleza maana ya urejeshi katika kitenzi. (b) Tunga sentensi tatu zinazoonesha urejeshi wa: (i) Mtenda nafsi ya tatu umoja. (ii) Mtendwa (idadi - wingi). (iii) Mtenda (kitu). 6. Andika maneno matano ambayo yameundwa kutokana na kufananisha sauti. Kwa kila nen sentensi moja. 7. (a) Eleza maana ya Kiambishi. (b) Bainisha viambishi vilivyopo katika vitenzi vifuatavyo: (i) Tunalima. (ii) Wanatembea. (iii) Godoro. Ukurasa wa 3 kati ya 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org SEHEMU C (Alama 10) UANDISHI Jibu swali moja (1) kutoka sehemu hii. 8. Andika insha isiyozidi maneno mia tatu (300) na isiyopungua mia mbili na hamsini (250) kuhusu faida za televisheni kwa jamii. 9. Umechaguliwa kutoa risala kwa niaba ya wanakijiji wa kijiji cha Kisombogho, wanaotaka kutoa shukrani zao kwa Mkuu wa Wilaya aliyewachimbia kisima cha maji kijijini hapo. Andika risala utakayoisoma siku ya kikao. SEHEMU D (Alama 10) MAENDELEO YA KISWAHILI Jibu swali la kumi (10) 10. Taasisi ya Elimu (TET) na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) ni miongoni mwa asasi zilizoanza mara tu baada ya uhuru. Fafanua kazi tatu kwa kila moja katika kukua na kuenea kwa Kiswahili nchini Tanzania. SEHEMU E (Alama 45) FASIHI KWA UJUMLA Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii. Swali la 15 ni la la ORODHA YA VITABU USHAIRI M.S. Khatibu (DUP) Wasakatonge - Malenga Wapya - TAKILUKI (DUP) Mashairi ya Chekacheka - T.A. Mvungi (EP & D.LTD) RIWAYA Ben J. Hanson (MBS) Takadini - Watoto wa Maman’tilie - E. Mbogo (H.P) Joka la Mdimu - A.J. Safari (H.P) TAMTHILIYA Steve Reynolds (MA) Orodha - Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe - E. Semzaba (ESC) Kilio Chetu - Medical Aid Foundation (TPH) 11. (a) Kwa kutumia mifano dhahiri, jadili muundo wa vitendawili kwa kutoa hoja muhimu (b) Fafanua dhima tatu za vitendawili kwa jamii. 12. "Mshairi ni mwalimu wa viongozi wa nchi." Jadili kauli hii kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma. Ukurasa wa 4 kati ya 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org 13. "Fasihi ya Kiswahili imemweka mwanamke katika hadhi tofauti tofauti." Thibitisha usemi huu kwa kutumia hoja tatu kwa kila riwaya kutoka katika riwaya mbili ulizosoma. 14. Kwa kutumia hoja tatu kwa kila tamthiliya kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma, jadili kufaulu kwa waandishi katika kipengele cha utumizi wa tamthali za semi. 15. (a) Visasili ni nini? (b) Tungakisasili kimoja kuhusu "Mnyama unayempenda." Ukurasa wa 5 kati ya 5