Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION EXAMINATION 021 KISWAHILI (Kwa Watahiniwa Walioko Shuleni tu) Muda: Saa 3 Jumanne, 05 Novemba 2013 mchana Maelekezo 1. Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E. 2. Jibu maswali yote katika sehemu A, B na D, swali moja (1)kutoka sehemu C na maswali matatu (3) kutoka sehemu E. Swali la 15ni la lazima. 3. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali. 4. Simu za mkononi haziruhusiwi katika chumba cha mtihani. 5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia. Ukurasa wa 1 kati ya kurasa 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org SEHEMU A (Alama 10) UFAHAMU Jibu maswali yote katika sehemu hii. 1. Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata: Baba alikuwa na wajibu maalum wa kuhakikisha usalama wa familia yake. Ilimbidi awe na nyumba watakamoishi mke na watoto. Nyumba zilijengwa kwa mitindo tofauti katika sehemu mbalimbali hapa nchini. Wanyakyusa walikuwa na ujenzi wao ambao ni tofauti na ule wa Wahaya. Wote wakijenga kwa ufundi wa kuvutia sana. Serikali yetu imehifadhi kwa njia ya makumbusho nyumba zilizojengwa na wakazi wa sehemu mbalimbali hapa nchini wakitumia mitindo yao ya asili. Nyumba hizi zipo katika kijiji cha makumbusho kilichopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Baba akishirikiana na mama walikuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa jamii yao ilipata chakula cha kutosha. Mapema watoto nao walishiriki katika shughuli za kutafuta na kuandaa chakula. Jamii nyingine hapa nchini zilikuwa zikishughulika na ufugaji tu. Maisha na utajiri wa jamii hizi ulitegemea wanyama. Tangu utoto wao, mafunzo makuu yalihusu ufugaji. Kwa mfano, mtoto wa kimasai alijifunza kuchunga na kulinda wanyama wake tangu utotoni. Ilimbidi awe askari hodari, aweze kupambana na maadui waliotaka kuteka wanyama wao. Alitakiwa aweze kupigana na wanyama wakali porini wenye kuishambulia mifugo. Kumuua simba ilikuwa ni ishara kubwa ya uhodari wa kijana wa kimasai. Mafunzo ya kumwandaa kijana huyo, tangu utoto wake kwa kazi zitakazomkabili katika maisha, yalichukua sehemu kubwa ya malezi. Kijana wa Kihaya alikabiliwa na mazingira tofauti sana na yale mwenzie wa kimasai. Wahaya ni wakulima, ufugaji ulichukua sehemu ndogo tu katika shughuli zao za kiuchumi. Wahaya hulima mazao ya kudumu kama vile migomba, mashamba yao yalihitaji ulinzi na utunzaji mzuri. Hivyo serikali imara yenye kuhakikisha amani katika nchi ili raia waweze kuendelea na kazi za kilimo kwa amani, ilihitajika. Pia Wahaya walihitaji nyumba za kudumu; maana hali ya maisha yao haikuruhusu uhamaji wa mara kwa mara kama vile Wamasai. Kwa hiyo mafunzo kamili yalihitajika ili kuwaandaa watoto kwa maisha ya namna hiyo. Maisha katika sehemu mbalimbali katika nchi yalilazimu ziwepo njia maalum za kuwalea, kuwafundisha na kuwaandaa kwa yale yatakayowakabili katika siku za usoni. Maswali (a) Eleza faida mbili zinazoweza kupatikana kwa kuhifadhi mitindo ya nyumba za asili katika kijiji cha makumbusho. (b) Unafikiri ni sababu gani iliifanya jamii ya Kimasai kuhamahama? (c) Kwa mujibu wa habari uliyoisoma vijana walikuwa na jukumu gani katika jamii zao? (d) Andika kichwa cha habari kisichozidi maneno matano kinachofaa kwa habari uliyoisoma. (e) Andika methali ya Kiswahili inayoendana na aya ya mwisho ya habari uliyoisoma. Ukurasa wa 2 kati ya kurasa 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org 2. Fupisha habari uliyoisoma kwa maneno yasiyozidi mia moja (100). SEHEMU B (Alama 25) SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA Jibu maswali yote katika sehemu hii. Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org 3. Onesha nomino katika tungo zifuatazo kisha bainisha ni aina gani ya nomino: (a) Hatuna budi kumshukuru Mola. (b) Mazao yamestawi shambani. (c) Uzalendo usisitizwe shuleni. (d) Mpeleke mtoto ndani. (e) Nimechoshwa na upweke. 4. Andika tungo zifuatazo kwa usahihi: (a) Mwenyekiti alihairisha kikao. (b) Mtoto amedumbukia shimoni. (c) Kila mwanafunzi anatakiwa kuchangia deksi. (d) Mama amenunua dazani ya sufuria. (e) Mwanafunzi msafi amepewa zawadi. 5. Tambulisha viambishi vyenye dhima zilizowekwa kwenye mabano katika maneno yafuatayo: (a) Hakukumbuka (njeo ya wakati uliopita) (b) Wamekamatana (kauli ya kutendana) (c) Akisema (hali ya masharti) (d) Ananiona (kurejesha mtendwa) (e) Tuliwashangilia (kurejesha watenda) (f) Huimba (hali ya mazoea) (g) Wamelima (wakati uliopita hali timilifu) (h) Wanatucheka (urejeshi wa watendwa) (i) Hawakusoma (ukanushi) (j) Amenipigisha (kauli ya kutendesha) 6. Onesha maana tano za neno “kata” na kwa kila maana tunga sentensi moja. 7. “Upatanisho wa kisarufi ni kigezo kimojawapo kati ya vigezo vya kuunda ngeli za nomino.” Thibitisha dai hilo kwa kutunga sentensi ukitumia ngeli zifuatazo: (a) U-I (b) LI-YA (c) U-ZI (d) I-ZI (e) U-YA Ukurasa wa 3 kati ya kurasa 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org SEHEMU C (Alama 10) UANDISHI Jibu swali moja (1) kutoka sehemu hii. 8. Wewe ni mfanyabiashara mashuhuri mjini Dodoma. Andika barua ya kutuma bidhaa kwa mteja wako aitwaye Dunia Msimbo anayeishi Lindi. Jina lako liwe Nyila Sasisha. 9. Andika tangazo kwenye gazeti la Rai ukitoa taarifa kuhusu kupotea kwa mwanao aitwaye Raha Karaha, jina lako liwe Furaha Machupa. SEHEMU D (Alama 10) MAENDELEO YA KISWAHILI Jibu swali la kumi (10) 10. Kwa kutumia hoja tano, onesha juhudi za Wajerumani katika kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili nchini wakati wa utawala wao. SEHEMU E (Alama 45) FASIHI KWA UJUMLA Jibu maswali matatu (3) kutoka sehemu hii. Swali la 15ni la lazima. 11. Fafanua matatizo matano ya kuhifadhi kazi za fasihi simulizi kwenye kanda za kunasa sauti. 12. “Mshairi siku zote hukemea uonevu katika jamii.” Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma. 13. “Fasihi ni chuo cha kufundisha maisha kwa jamii husika. “Jadili ukweli wa kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila riwaya kati ya riwaya mbili ulizosoma. 14. Chagua wahusika watatu wa kike, kutoka katika kila tamthiliya kati ya tamthiliya mbili ulizosoma, kisha onesha kukubalika kwao kama kielelezo cha maisha katika jamii. 15. Tunga tenzi yenye beti tano kuhusu ongezeko la watoto wa mitaani. Ukurasa wa 4 kati ya kurasa 5
Mtihani huu na mitihani mingine inapatikana kwenye tovuti yetu: http://maktaba.tetea.org ORODHA YA VITABU Ushairi Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP) Malenga wapya - TAKILUKI (DUP) Mashairi ya Chekacheka - T.A Mvungi (EP& D.LTD) Riwaya Takadini - Ben Hanson (MBS) Watoto wa mama N’tilie - E. Mbogo (H.P) Joka la Mdimu - A.J. Safari (H.P.) Tamthiliya Orodha - Steve Reynolds (MA) Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe - E. Semzaba (ESC) Kilio Chetu - Medical Aid Foundation (TPH) Ukurasa wa 5 kati ya kurasa 5